STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 26, 2014

Kuziona Yanga na Al Ahly Buku 7 tu

http://gatemedia.ahram.org.eg/english/News/2012/10/29/2012-634871100531794113-179.jpg
Al Ahly ya Misri
Yanga ya Tanzania
WAKATI Al Ahly wakitua nchini leo, viingilio vya pambano mkondo wa kwanza raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya watetezi hao kutoka Misri na Yanga litakalofanyika Jumamosi hii uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku kile cha chini kabisa kitakuwa ni Sh. 7,000.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Yanga ni kwamba watu watakaoketi jukwaa la viti vya rangi ya Chungwa, wakati VIP A tiketi moja itauzwa kwa Sh. 35,000 na kwa viti vya VIP B na C Sh. 25,000.
Na kwamba wapinzani wa yaani Al Ahly wanatarajiwa kuwasili asubuhi hii na watafikia katika hoteli ya Hyatt Regency, Kempinsky au Kilimanjaro Hotel, iliyopo maeneo ya Kivukoni.
Waarabu hao wanaweza kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gymkhana, uliopo kando ya bahari ya Hindi na kikosi wanachotarajiwa kuja nacho Dar es Salaam ni makipa; Sherif Ekramy, Ahmed Adel Abdel-Monem na Mahmoud Abou El-Sooud.
Mabeki ni; Wael Gomaa, Sherif Abdel-Fadil, Ahmed Fathi, Mohamed Naguib, Saad El-Din Samir, Sayed Moawad na Ahmed Shedid Qenawy.
Viungo ni; Hossam Ashour, Shehab El-Den Ahmed, Ahmed Nabil Manga, Ahmed Shokry, Mahmoud ‘Trezeguet’, Rami Rabia, Walid Soliman, Abdullah El-Said na Mohamed Abou-Treika na washambuliaji El-Sayed Hamdy, Dominique  Da Silva, Emad Meteb na Amr Gamal ambaye ndiye tegemeo la mabao la timu hiyo kwa sasa.

No comments:

Post a Comment