STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 26, 2014

Ivo Mapunda apatwa pigo zito, afiwa na baba

KIPA namba moja Tanzania, Ivon Philip Mapunda amefiwa na baba yake mzazi Mzee Philip Mapunda jana jioni na anatarajiwa kuzikwa kesho kijijini kwao, Tukuyu Mbeya.
Kipa huyo wa Simba SC, Ivo ameiambia BIN ZUBEIRY leo asubuhi kwamba, Mzee Mapunda aliyekuwa ana umri wa miaka 86 amefariki akiwa katika hospitali ya Ikonda, iliyopo Njombe ambako alikuwa amelazwa kwa takriban miezi miwili na nusu.
Pole mpiganaji; Ivo Mapunda amefiwa na baba yake mzazi jana 

Ivo alisema Mzee Mapunda alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kibofu cha mkojo, sukari na vidonda vya tumbo. 
Ivo aliyekuwa akizungumza akiwa njiani kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam, amesema mwili wa marehemu kwa sasa upo kijijini Tukuyu tangu usiku wa jana. Pole Ivo na famili yake. Mungu ampumzishe kwa amani Mzee Mapunda.
BIN ZUBEIRY

No comments:

Post a Comment