STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 26, 2014

Yanga wapo kamili kuiua Al Ahly Jumamosi

Tegemeo la Tanzania michuano ya Afrika kwa sasa, Yanga
WAWAKILISHI pekee  wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga imeingia kambini katika hotel ya Laico Ledger iliyopo eneo la Bahari Bahari Beach Kunduchi  tayari kwa ajili ya pambano la Jumamosi dhidi ya ya Al Ahly kutoka Misri.
Mchezo huo wa Yanga dhidi ya Al Ahly utachezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisa Habari wa Yanga Baraka Kizuguto alisema kikosi cha Yanga  chenye wachezaji 25 pamoja na benchi la Ufundi kilianza mazoezi juzi jioni katika Uwanja wa Kaunda Makao Makuu ya Klabu na jana asubuhi kimeendelea kujinoa katika Uwanja wa Boko Beach.
“Wachezaji wote wapo katika hali nzuri, mpaka sasa hakuna mchezaji majeruhi kuelekea mchezo huo,”alisema.

Alisema  Kocha  anatambua mchezo huo utakua ni mgumu, kwani Al Ahly wana uzoefu na michezo ya kimataifa lakini na wao wana malengo na zaidi  ni kufanya mapinduzi kwa kushinda
“Kwa vile Kocha anawafahamu Al Ahly  vizuri hakuna kitakachoshindikana kwasababu tayari tumepata  mbinu zao kutoka kwa  Kocha Msaidizi Boniface Mkwasa, kilichobaki ni kuwaandaa wachezaji kiakili,”alisema.

Katika mchezo huo, Mshambuliaji wa Kimataifa Emanuel Okwi atakuwa ni miongoni mwa wachezaji tegemeo katika kikosi kitakachotua dimbani siku hiyo. Kizuguto alithibitisha ushiriki huo kwa kuonyesha leseni yake iliyotoka Shirikisho la Soka Afrika(CAF) .



Al Ahly imewasili leo alfajiri saa 12 kasorobo kwa Shirika la Ndege la Misri Egypt Air kikiwa na watu 35 wakiwemo wachezaji 22, bechi la Ufundi 8 pamoja na viongozi 5 na wamefikia katika Hotel ya Hyatt Kempsinki ambapo ndio itakuwa ikiweka kambi.

Siku ya Jumatano na Alhamisi  jioni watafanya mazoezi katika Uwanja wa IST uliopo Upanga, na Ijumaa jioni watapata fursa ya kufanya mazoezi katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam tayari kwa mchezo huo wa Jumamosi.


Tiketi zitauzwa kwenye vituo mbalimbali kuanzia Ijumaa ambapo kiingilio cha juu ni  Shs 35,000,  25,000,  13,000 na cha chini kwa viti vya kijani na bluu ni Sh. 7000.

Rekodi ya Al Ahly:
Wana mataji 19 moja zaidi ya mataji 18 ya Ac Milan
Imeshinda mara 8 kombe la mabingwa barani Afrika, mwaka 1982,1987,2001,2005,2006, 2008, 2012, na 2013. Makombe 4 ni ubingwa wa Kombe la washindi 1984,1985,1986, 1993.

Mara sita imetwaa kombe la CAF Super Cup 2002, 2006,2007,2009, 2013, na 2014 na mmoja likiwa la Afro-Asian Cup mwaka 1988.

No comments:

Post a Comment