STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 8, 2014

Chelsea yapaa kileleni, Arsenal majanga matupu Anfield

Hazard akishangilia moja ya mabao yake matatu leo
Martin Skrtel akishangilia moja ya mabao yake ya leo yaliyoiangamiza Arsenal
WAKATI Arsenal wakipata aibu ugenini kwa kunyonyolewa mabao 5-1 na Liverpool, Chelsea imetupia nafasi kwa kupta ushindi nyumbani kwa kuilaza Newcastle United kwa mabao 3-0 na kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu ya England.
Mabao matatu (hat-trick) ya Eden Hazard katika dakika ya 27, 34 na jingine la mkwaju wa penati kipindi cha pilli yalitosha kuwapeleka vijana wa kocha Jose Mourinho hadi kileleni ikiziporomosha Arsenal na Manchester City zilizokuwa juu yake baada ya timu hizo kuwa na matokeo yasiyovutia leo.
Arsenal ikisafiri hadi Anfield ilikumbana na kipigo cha aibu cha mabao 5-1 toka kwa wenyeji wao Liverpool huku Man City ikilazimishwa suluhu na Norwich City.
Liverpool ilipata ushindi wake kwa mabao mawili ya Martin Skrtel na  Raheem Sterling na jingine moja la  Daniel Sturridge yalitosha kuiangamiza Arsenal iliyopata bao la kufutia machozi kwa penati ya Mikel Arteta.
Katika mechi nyingine zilizochezwa leo, Aston Villa imelala 2-0 mbele ya West Ham United, huku Crystal Palace ikiilaza West Brom mabao 3-1, Southampton ikilazimishwa sare nyumbani na Stoke City kwa kufunga mabao 2-2 na Hull City kuizima Sunderland kwa mabao 2-0 na mechi iliyoisha hivi punde Swansea City imepata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Cardiff kwa kuilaza mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment