STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 14, 2014

Hassan Vocha kuwa Surprise mashabiki leo

 
MUIMBAJI mpya wa kundi la taarab lililorejea upya la Dar Modern 'Wana wa Jiji', Hassan Vocha, amewaahidi kuwafanyia 'mshangao' mashabiki wa kundi hilo watakaohudhuria utambulisho wake na wasanii wenzake unaofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Vocha na waimbaji wenzake kadhaa walionyakuliwa na kundi hilo lililowahi kutamba na vibao kama 'Pembe la Ng'ombe', 'Kitu Mapenzi' na 'Malavidavi' watatambulishwa leo 'Valantine Day' eneo la Magomeni.
Akizungumza na MICHARAZO, msanii huyo alisema ameandaa kitu 'spesho' kwa mashabiki wa muziki wa taarab katika onyesho hilo maalum.
"Kuna kitu maalum nimewaandalia mashabiki kwa ajili ya utambulisho huo ikizingatiwa onyesho litafanyika Siku ya Wapendanao', naomba waje ukumbini kujua kitu gani hicho," alisema Vocha.
Vocha aliyejipatia umaarufu mkubwa kupitia wimbo wake wenye jina hilo la 'Vocha' alichoimba na Dogo Aslay wakati akiwa Mkubwa na Wanae, alisema jukumu alililopewa kuvaa 'viatu' vya Hammer Q ni changamoto kwake.
"Najua ni changamoto kwangu, lakini kwa vile mimi ni msanii mwenye kipaji nitawapa burudani mashabiki wenye imani nami," alisema Vocha ambaye katika onyesho hilo ataimba karibu nyimbo zote alizoimba Hammer Q.
Uzinduzi huo wa Dar Modern utafanyika Travertine Hotel na kusindikizwa na makundi ya Kibao Kata na Baikoko ambapo Vocha atatambulisha nyimbo mbili alizorekodi katika albamu za kundi hilo za 'Oh My Sweet' na 'Ngoma Inapasuka'.

No comments:

Post a Comment