STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 14, 2014

Juan Mata afunguka kuhusu Mashetani Wekundu


368919_heroa
Mchezaji ghali zaidi kuwahi kununuliwa na klabu ya Manchester  United, Juan Mata amesisitiza kwamba ana furaha kucheza kwenye sehemu wowote uwanjani atakayopangwa na mwalimu wake na amebakia mtu mwenye furaha tangu alipojiunga na klabu hiyo mwezi uliopita.

Mhispania huyo ambaye amecheza mechi zote nne tangu alipojiunga na timu, na ameiwezesha timu yake kufunga mabao matatu na kuhakikisha inapata pointi 5, huku akichezeshwa kwenye namba tofauti na kocha David Moyes.
Moyes ameshamchezesha Mata kwenye winga zote mbili, amecheza nyuma ya mshambuliaji, lakini kiungo huyo mwenye miaka 25 hana chaguo lolote la sehemu ya kuchezeshwa anachojali ni kuisadia timu yake kushinda.
“Maisha yangu yote ya soka nimekuwa nikicheza upande wa kushoto, kulia na nyuma ya mshambuliaji,” Mata aliwaambia waandishi wa habari.
“Sijali wapi nachezeshwa na kocha wangu. Nina furaha nipo kwenye klabu kubwa sana na nina matumaini tutamaliza msimu vizuri.
“David de Gea amenisaidia kupazoea hapa, pia Chicharito, [Antonio] Valencia, na Rafael, wote wanaongea kihispania na wamenisaidia.”

No comments:

Post a Comment