STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 19, 2014

Prisons yaigagadua JKT Ruvu 6-0


Prisons
MABINGWA wa zamani wa Tanzania, Prisons ya Mbeya jioni ya leo imetoa kisago cha aina yake kwa maafande wenzao wa JKT Ruvu kwa kuitandika mabao 6-0 katika pambano pekee la Ligi Kuu Tanzania Bara lililochezwa nchini leo.
Pambano hilo limechezwa kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya ambapo mechi hiyo ya 'kiporo' ilishuhudia wenyeji wakipata mabo yao kupitia kwa Peter Michael aliyefunga mabao mawili, Omega Seme, Nurdin Chona, Lugano Mwangama na Frank William na kuiwezesha timu hiyo kuchupa hadi nafasi ya 9 ikiwa na pointi 19 sawa na JKT wanaoshuka hadi nafasi ya 10 kuipisha Prisons kwa tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa.
Kipigo hicho kinaweza kuwa mwanzo mbaya kwa JKT inayojiandaa kushuka dimbani Jumapili dhidi ya Simba, ikiwa chini ya kocha mpya Fred Minziro baada ya aliyekuwa kocha wao Mbwana Makatta kubwaga manyanga wiki chache zilizopita.
Timu hiyo katika mechi nne zilizopita imeambulia pointi moja tu baada ya kufungwa mechi tatu na kupata sare mchezo mmoja dhidi ya Oljoro JKT.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara:
                          P    W     D     L      F     A   GD  PTS
01.Azam            16   10    06   00   29   10   19  36
02.Yanga           16   10    05   01   34   12   22  35
03.Mbeya City    18   09    08   01   24   14   10  35
04.Simba           18   08    08   02   33   16   17  32
05.Ruvu Sh.       18   06    07   05   20   19   01  25
06.Kagera Sugar 18  05    08   05   15    15   00  23
07.Coastal Union18   04    10    04  12    09   03  22
08.Mtibwa Sugar 18   05    07    06  21   22  -01  22
09.Prisons          17   04    07    05   15   16  -01 19
10. JKT Ruvu      18   06    01    11   13   27  -14 19
11.Mgambo        18   04    05    09    10  26 -16  17
12.Oljoro            19   02    09    08    14  28 -14  15
13.Ashanti          17   03    05    09   14   28 -16  14
14.Rhino Rangers18   02    07    09   12  22 -10  13
Wafungaji:14- Tambwe Amisi (Simba)
09- Elias Maguri (Ruvu Shooting), Kipre Tchetche (Azam)
08- Hamis Kiiza (Yanga), Juma Luizio (Mtibwa Sugar)
06- Themi Felix (Kagera Sugar), Mrisho Ngassa, Didier Kavumbagu (Yanga), Peter Michael (Prisons)
05- Tumba Sued (Ashanti Utd), Jerry Santo (Coastal Union), Jerome Lambele (Ruvu Shooting)
04- Jerry Tegete (Yanga), Jonas Mkude, Betram Mombeki (Simba), Bakar Kondo, Salum Machaku (JKT Ruvu),
03- Haruna Chanongo, Ramadhani Singano (Simba), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu), Humphrey Mieno, Mcha Khamis (Azam), Amir Omary (Oljoro), Jeremia John (Mbeya City), Said Dilunga (Ruvu Shooting)


Mechi zijazo za Ligi hiyo wikiendi hii;
Feb 22, 2014
Ruvu Shooting  vs Yanga SC
Kagera Sugar  vs Rhino
Mtibwa Sugar  vs Ashanti Utd
Coastal Union vs Mbeya City
JKT Oljoro  vs Mgambo
Azam   vs Prisons
 

Feb 23, 2014
Simba SC    vs JKT Ruvu

No comments:

Post a Comment