STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 2, 2011

Zanzibar mguu ndani mguu nje Kombe la Chalenji 2011



HATMA ya timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes kuendelea na michuano ya Kombe la Chalenji, inasubiri majaliwa ya sheria ya kumpata best losser, kufuatia goli la Amissi Cedric lililo wapa ushindi Burundi wa goli 1-0 pala walipowakabili Uganda jana.
Zanzibar ilipata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano hiyo inayoendelea jijini jana katika pambano lililochezwa mapema kwenye uwanja wa Taifa kwa kuilazaq Somalia mabao 3-0 na kufikisha pointi nne.
Mabao ya mshambuliaji wao hatari Suleiman Kassim 'Selembe', Ally Badru na nahodha Aggrey Morris yaliisaidia Zanzibar kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kutegemeana na matokeo ya makundi mengine yanayochezwa leo na kesho.
Kama mambo yatajipa Zanzibar waliopo nafasi ya tatu katika kundi lao la B nyuma ya Burundi wanaoongoza kwa pointi 7 na Uganda wenye pointi sita itafuzu hatua ya robo fainali.
Kwani kama sio ushindi wa bao 1-0 iliyopata Burundi mbele ya Uganda, Zanzibar isingekuwa na wakati mgumu wa kusubiri kapu la hisani kusonga mbele.
Zanzibar itabidi wangoje hekima za CECAFA kama watapata nafasi katika best loser ingawa kwa kuangalia matokeo ya makundi mengine yalivyo moja ya nafasi ya mshindwa bora kwa 'mashujaa' hao wa Zanzibar ni kubwa, ingawa soka halipo hivyo.
Ndugu zao Tanzania kesho nao watakuwa vitani kupigana kutinga robo fainali, kwa kuumana na Zimbabwe wanaolingana nao pointi tatu, huku Rwanda amabyo itacheza leo dhidi ya Djibout ikiwa imeshajihakikishia nafasi mojawapo ya kucheza hatua hiyo ya mtoani itakayoanza Jumatatu.

1 comment:

  1. This blog very interesting but you can also try these ..www.jigambeads.com and ..www.tanzaniakwetu.com for popularity and more advert to advertise. Thanks

    ReplyDelete