STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 27, 2011

Maneno, Matumla washindwa kutambiana





MABONDIA wakongwe wa ngumi za kulipwa nchini, Maneno Oswald 'Mtambo wa Gongo' na Rashid Matumla 'Snake Man' juzi walishindwa kutambiana baada ya pambano lao la kumaliza ubishi kuisha kwa kutoka sare.
Hata hivyo Oswald, ameyakubali matokeo hayo kwa ushingo upande, akidai kwamba alistahili kutangazwa mshindi kutokana na kumzidi maarifa mpinzani wake aliyeteleza na kuanguka ulingoni mara sita na kujikuta akiumia mguu.
Pambano hilo lisilo la ubingwa lililokuwa na raundi 10 na uzani wa kati lililosimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Nchini, PST, lilifanyika kwenye ukumbi wa Heinken Pub, Mtoni Kijichi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Katika pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi wa kimataifa wa mchezo huo nchini, Anthony Rutta, mabondia wote wawili walipewa pointi 99-99, kitu ambacho Maneno Oswald aliiambia MICHARAZO kuwa ni kama mpinzani wake 'alibebwa' tu.
"Kwa kweli nimeyakubali matokeo hayo kwa shingo upande kwa vile nilistahili kabisa ushindi, ila mpinzani wangu amelindwa, Matumla kaanguka mara sita ulingoni, utetezi wake ulingo ulikuwa unateleza mbona mie sikuteleza," alisema Maneno.
Aliongeza kuwa, licha ya kuambiwa kuna mipango inafanywa ili warudiane tena, yeye binafsi hana mpango wa kufanya hivyo na kudai anataka kupigana na Mada Maugo, aliyedai ndiye anayemuona mpinzani wake wa ukweli.
"Sitarudiana na Matumla hata iweje, nataka kupigana na Maugo kwani namuona ndiye bondia wa kweli kwa sasa nchini katika uzito wetu.," alisema.
MICHARAZO lilijaribu kumsaka Matumla kusikia kauli yake juu ya matokeo ya mchezo huo, lakini simu yake haikuwa hewani.
Hilo lilikuwa ni pambano la nne kwa Maneno na Matumla kuzipiga, kwani walishacheza mechi tatu na mara mbili Matumla aliibuka na ushindi dhidi ya moja la mpinzani wake.
Katika mechi nyingine za utangulizi zilizochezwa kabla ya pambano la wawili, Ubwa
Kabla ya pambano hilo kuchezwa kulifanyika mechi kadhaa za utangulizi, ambapo moja wao lilimkutanisha bondia Ubwa Salum aliyempiga kwa pointi Mustafa Dotto.

No comments:

Post a Comment