STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 27, 2011

Kingwande 'aitabiria' mema Lyon duru la pili

KIUNGO Mshambuliaji nyota wa timu ya African Lyon, Adam Kingwande, amesema ana matumaini makubwa kwa timu yake kufanya vema katika duru lijalo la Ligi Kuu Tanzania Bara kutokana na kusajiliwa kwa wchezaji kadhaa wapya katika kikosi chao.
Akizungumza na MICHARAZO, Kingwande, aliyewahi kuzichezea timu za Ashanti Utd na Simba, alisema usajili uliofanywa kupitia dirisha dogo lililomalizika mwezi uliopita kwa namna moja utaisaidia timu yao kufanye vema kwenye duru hilo lijalo.
Kingwande, alisema awali kikosi chao kilikuwa na mapungufu makubwa ambayo yaliifanya Lyon iyumbe kwenye duru la kwanza, jambo ambalo lilionwa na kufanyiwa kazi na uongozi na benchi la ufundi lao la ufundi kwa kusajiliwa wachezaji hao wapya.
Alisema kwa namna usajili huo uliofanyika kwa kuchanganya wachezaji wa ndani na nje ya nchi ni wazi Lyon, itakuwa moto wa kuotea mbali katika duru lijalo, kitu alichotaka timu pinzani zikae chonjo dhidi yao.
"Binafsi naamini Lyon itakuwa moto duru lijalo kutokana na kuongezwa wachezaji wapya kupitia dirisha dogo, pia, nashukuru kwamba kwa sasa nipo fiti tukianza maandalizi ya duru hilo," alisema.
Lyon inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa tatu sasa, ilianza vema duru la kwanza kabla ya kutetereka ikimaliza duru hilo ikiwa nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi hiyo kwa kujikusanyia jumla ya pointi 14.
Msimamo wa ligi hiyo unaongozwa na Simba yenye pointi 28 ikifuatiwa na Yanga yenye piinti 27 na Azam waliona pointi 23 sawa na JKT Oljoro wanaoshika nafasi ya nne.

Mwisho

No comments:

Post a Comment