STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 27, 2011

Mchaki 'aula' VIlla Squad

KLABU ya soka ya Villa Squad, imemteua aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka wilaya ya Kinondoni, KIFA, Frank Mchaki kuwa Kaimu Katibu Mkuu baada ya Katibu Mkuu wao, Idd Godigodi kuwa mgonjwa.
Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ramadhani Uledi, aliiambia MICHARAZO kuwa, wamelazimika kumuomba Mchaki awashikie nafasi hiyo ya Ukatibu kuitokana na Katibu wao kuwa mgonjwa na huku wakikabiliwa na majukumu kabla ya kuanza kwa ligi.
Uledi, alisema kamati yao ya utendaji ililazimika kuhitisha kikao cha dharura na kufanya maamuzi hayo, kwa nia ya kuifanya Villa isitetereke wakati ikijiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania bara litakaloanza Januari 21.
"Tumemundikia barua kumuomba akaimu ukatibu mkuu, kutokana na uzoefu alionao na ametukubalia kwani kabla ya uteuzi alikuwa ndiye Katibu wa Kamati ya Usajili ya klabu yetu ambayo alifanya kazi nzuri kwa kuimarisha kikosi," alisema Uledi.
MICHARAZO iliwasiliana na Mchaki, ambaye alikiri kuombwa na uongozi wa klabu hiyo kushikilia cheo hicho na kudai haoni sababu ya kuikataa ilihali ni mmoja wa wadau wakubwa wa klabu hiyo.
"Ni kweli kuhusu jambo hilo na nimeshawajibu kuafiki uteuzi huo na kuwahidi wana Villa wanipe ushirikiano kuiwezesha timu yetu ifanye vema kwenye ligi hiyo na kuondokanan na janga la kushuka daraja pamoja na ukata uliopitiliza," alisema.
Villa Squad iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, ndiyo inayoshikilia mkia katika msimamo wa ligi hiyo yenye timu 14.

Mwisho

No comments:

Post a Comment