STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 2, 2011

Sikinde yajiandaa kukamilisha albmu mpya

BENDI kongwe ya Mlimani Park 'Sikinde' ipo katika maandalizi ya mwisho ya kufyatua albamu yao mpya itakayozinduliwa mwishoni mwa mwezi ujao.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema kuwa tayari wameshafyatua vibao kadhaa kwa ajili ya albamu hiyo itakayokuwa na nyimbo sita na watamalizia nyimbo zilizosalia kabla ya katikati ya Desemba.
Milambo, alisema katika harakati za kuitambulisha albamu hiyo wamefyatua video ya kibao chao cha 'Jinamizi la Talaka' ambao unatesa kwenye vituo kadhaa vya redio nchini.
"Sikinde tupo katika maandalizi ya kukamilisha kurekodi albamu yetu mpya itakayokuwa na nyimbo sita, ambayo tutaitoa hadharani mwishoni mwa Desemba," alisema.
Katibu huyo alivitaja baadhi ya vibao vitakavyokuwa katika albamu hiyo itakayochukua nafasi ya 'Supu Imetiwa Nazi' kuwa ni; 'Jinamizi la Talaka', 'Bundi', 'Mihangaiko ya Kazi' na 'Asali na Shubiri'.
Sikinde, kwa muda wa miaka miwili sasa haijatoa albamu yoyote tangu ilipotamba na Supu Imetiwa Nazi ambayo ilifyatuliwa wakati ikiwa chini ya Shirika na Maendeleo Dar es Salaam, DDC iliyowatema rasmi mapema mwaka uliopita.

No comments:

Post a Comment