STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 2, 2011

Poulsen bado hajaniamini-Jabu




BEKI mahiri wa Simba anayezichezea pia timu za taifa, Juma Jabu, amekiri kwamba kocha wa sasa wa timu ya taifa (Taifa Stars), Jan Poulsen hajamuamini ndiyo maana amekuwa haitwi mara kwa mara katika kikosi hicho.
Hata hivyo, alisema kutoaminiwa huko kunatokana na kuwepo majeruhi kwa muda mrefu tangu Mdenmark huyo alipoitwaa timu hiyo toka kwa Mbrazil, Marcio Maximo.
Jabu maarufu kama 'JJ', alisema amekuwa akipata nafasi ndogo ndani ya kikosi cha Stars kwa vile Poulsen hajaridhika naye, tofauti na ilivyo kwa Maximo ambapo panga pangua hakukosekana kikosini.
"Sio siri sijapata nafasi kubwa ndani ya kikosi cha Stars tangu iwe chini ya Poulsen, hii inatokana na kocha kutoniamini pengine kwa vile nilikuwa majeruhi na hivyo kutoonekana dimbani, ila naamini michuano ya Chalenji itanirejesha Stars," alisema.
Alisema kuitwa kwake katika kikosi cha Kilimanjaro Stars ambayo leo inamaliza mechi zake za makundi dhidi ya Zimbambwe, ni fursa nzuri ya kumshawishi Poulsen ampe nafasi ya kudumu katika Stars inayokabiliwa na mechi za kuwania kufuzu CAN 2013 na WC 2014.
Katika hatua nyingine beki huyo alisema mipango yake ya kwenda kucheza soka la kulipwa nchini Afrika Kusini inaendelea vema, ingawa hakupenda kuweka bayana kwa madai suala lake linasimamiwa na wakala wake.
"Mipango yangu ya kwenda Afrika Kusini ipo pazuri, ila mwenye nafasi ya kuliongelea kwa undani ni wakala wangu," alisema Jabu.

No comments:

Post a Comment