STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 2, 2011

Mkenya Kariuki kutua nchini Kesho kupiogana na Nassib Ramadhan



MPINZANI wa Bingwa wa Dunia anayetambuliwa na World Boxing Forum, Nassib Ramadhan 'Manny Pacquiao', Mkenya Anthony Kariuki, anatarajia kutua nchini kesho kwa pambano lao litakalofanyika Desemba 9 jijini Dar es Salaam.
Kariuki na Nassib watapigana katika pambano lisilo la ubingwa la raundi 10 uzani wa Fly kwenye ukumbi wa DDC Keko, ambapo watasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Akizungumza na MICHARAZO, mratibu wa pambano hilo, Pius Agathon, alisema Kariuki atatua nchini leo mchana akiambatana na kocha wake tayari kwa pambano lake ambalo litaenda sambamba na maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru.Agathon, alisema kambi ya Mkenya huyo itakuwa eneo la Keko, wakati mpinzani wake ipo eneo la Mabibo chini ya kocha wake, Christopher Mzazi.
"Mkenya atakayepigana na Nassib Ramadhan atatua nchini Jumamosi (kesho)na moja kwa moja ataingia kambini eneo la Keko, tayari kuvaana na mpinzani wake aliyejichimbia Mabibo," alisema Agathon.
Agathon aliongeza kuwa maandalizi kwa ujumla ya pambano hilo litakalohudhuriwa pia na nyota wa zamani wa mchezo huo walioliletea sifa Tanzania katika miaka 50 ya Uhuru yamekamilika na inasubiriwa siku ya kufanyika kwa mchezo huo.
Alisema siku hiyo kutakuwa na michezo mitano ya utangulizi kabla ya Nassib Ramadhan kupeperusha bendera ya Tanzania mbele ya Mkenya.

No comments:

Post a Comment