STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 17, 2014

16 kambi ya Maboresho waula Taifa Stars

Na Mwandishi Wetu, Mbeya
JUMLA ya wachezaji 16 wa kikosi cha Maboresho ya Timu ya Taifa(Taifa Stars) wamechaguliwa kujiunga na timu ya Taifa kwa ajili ya mechi za kirafiki kutoka kambi ya wachezaji 34 iliyokuwa Chuo cha Ualimu Tukuyu Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
Kikosi hicho  kimetangazwa leo na Kocha Msaidizi, Salum Mayanga, aliyekuwa na timu hiyo katika Mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hill View iliyopo jijini Mbeya.
Mayanga aliwataja wachezaji hao kuwa ni Mlinda mlango Benedict Mlekwa kutoka Mara, Walinzi wa kati ni Emma Simwanda kutoka Temeke na Joram  Mgeveja kutoka Iringa.
Walinzi wa pembeni ni Omari Kindamba wa Temeke, Edward Mayunga wa Kaskazini Pemba na Shirazy Sozigwa wa Ilala, viungo ni Yusufu Mlipili, Said Juma Ally kutoka Mjini Magharibi, Abubakar Mohamed wa Kusini Unguja na Hashimu Magona kutoka Shinyanga.
Viungo wa pembeni ni Omari Nyenje wa Mtwara na Chunga Zito kutoka Manyara.
Washambuliaji ni Mohammed Said kutoka Kusini Pemba, Ayubu Lipati wa Ilala, Abdurahman Othman  kutoka Mjini Magharibi na Paul Bundara kutoka Ilala.
Aliongeza, katika kikosi hicho pia wamejumuishwa wachezaji wawili waliojiunga na Timu ya Taifa ya vijana  U20; Mbwana Mshindo kutoka Tanga na Bayaga Fabian kutoka Mbeya.
Manyanga alisema wachezaji wengine walioachwa wataendelea kuwa kwenye uangalizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu(TFF) kwa sababu mpango wa maboresho ya timu ya Taifa ni endelevu.
Alisema Kambi ya timu hiyo iliyoanza Machi 22, imehitimishwa leo Aprili 17 kwa awamu ya kwanza ambapo wachezaji hao watajiunga na kikosi cha Stars mechi ya Kirafiki kisha watarudi tena wilayani Rungwe kwa ajili ya Kambi ya awamu ya Pili.

No comments:

Post a Comment