STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 17, 2014

Bale akifunga bao la ushindi la Real Madrid jana
BAO lililofungwa kiufundi kwa juhudi binafsi za Gareth Bale zimeiwezesha Real Madrid kunyakua taji la kwanza kwa msimu huu kwa kuilaza Barcelona katika mchezo wa fainali ya Kobe la Mfalme.
Mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa  Mestalla mjini Valencia, Hispania, ilikuwa ya kusisimua na Real Madrid waliwafunika wapinzani wao, licha ya wenyewe kumiliki sehemu mkubwa wa pambano hilo.
Real walianza kuandika bao  la kuongoza katika dakika ya 11, mfungaji Angel di Maria akimalizia pasi ya Karim Benzema, lakini Bartra akaisawazishia Barca dakika ya 68 kwa pasi ya Xavi.
Dakika tano kabla ya pambano hilo kumalizika nyota wa Wales, Gareth Bale aliyefunga bao la ushindi dakika ya 85 kwa pasi ya Fabio Coentrao na kumkimbiza beki wa Barcelona aliyemuondoka kwenye mstari kabla ya kuzidiwa mbio na kufunga bao maridadi lililompa Carlo Ancelotte furaha ya aina yake.
Katika mchezo huo, Mwanasoka bora wa dunia, Cristiano Ronaldo alikuwa nje leo akiendelea kuugulia maumivu yake na aliungana na wenzake kuwapongeza baada ya mechi kwa ushindi huo.
Baada ya kunyakua taji la kwanza msimu huu, Real sasa inaelekeza nguvu zake katika mataji mengine mawili, La Liga na Ligi ya Mabingwa ambako imefika hatua ya Nusu Fainali na itamenyana na mabingwa watetezi, Bayern Munich.
Kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Hispania, Real inachuana na Atletico Madrid walio kileleni na Barca walio nafasi ya tatu. 

No comments:

Post a Comment