STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 14, 2014

Lyon yaidonyoa PSG kimoja Ufaransa

Mfungaji wa bao pekee la Lyon, Ferri (12) akipambana uwanjani dhidi ya PSG jana
MABINGWA watetezi wa Ligi ya Ufaransa, PSG jana ilionja kipigo chake cha kwanza baada ya mfululizo wa ushindi katika ligi hiyo kwa kudonyolewa goli 1-0 dhidi ya Olympique Lyon.
Ikicheza ugenini, PSG ilishindwa kufuruka kwa Lyon waliopata bao lao katika dakika ya 31 kupitia kwa Jordan Ferri.
Pamoja na kwamba kipigo hicho hakijaiteteresha matajiri hao wa Paris, lakini imefanya pengo la pointi baina ya wapinzani wanaowafukuzia kileleni, Monaco kuwa pointi 10 badala ya 13 ya awali baada ya Monaco kupata ushindi ugenini siku ya Jumamosi dhidi ya Rennes.
PSG imeendelea kusaliwa na pointi zake 79, huku Monaco wakiwa nafasi ya pili na pointi zao 69 huku timu zote zikiwa zimecheza michezo 33 na kusaliwa na mechi tano kabla ya kufungia msimu wa 2013-2014.

No comments:

Post a Comment