STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 14, 2014

Bomu jingine lalipuka jijini Arusha

Kijana ambaye hakufahamika jina lake baada ya kupata majeraha makubwa mguuni.

Hali ya sintofahamu iliyowakumba wakazi wa jiji la Arusha baada ya bomu kulipuka jana.
Majeruhi baada ya bomu kulipuka.
Mmoja wa majeruhi akiwa hoi baada ya mlipuko.
Taarifa kutoka mjini Arusha zinasema bomu la kutengenezwa kwa mkono lililipuliwa jana usiku April 13 kwenye Baada iitwayo Arusha Night Park, iliyopo eneo la Mianzini jijin i Arusha na kusababisha watu kadhaa kujeruhiwa, huku taarifa zingine zikisema watu wawili wamepoteza maisha katika mlipuko huo kwamba ni watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Inaelezwa watu 15 walithibitishwa kuumia katika mlipuko huo wa tatu kutokea mkoani humo kwa kipindi cha mwaka mmoja baada ya tukio la mlipuko kanisani na kwenye mkutano wa CHADEMA na kupelekea vifo vya watu kadhaa.
Inaelezwa wengi wa majeruhi katika mlipuko huo wa jana ni wahudumu wa baa hiyo pamoja na waliojitokeza kuangalia mpira kqwenye truninga na kwamba walikimbizwa hospitali za Mount Meru, Seliani na St. Elizabeth kwa ajili ya matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment