STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 14, 2014

Man City yapata pigo kwa Yaya Toure

KLABU ya Manchester City imepata pigo baada ya kufahamika kuwa huenda kiungo wake mahiri Yaya Toure asicheze tena msimu huu baada ya kuumia katika mchezo dhidi ya Liverpool uliochezwa mwishoni mwa wiki katika Uwanja wa Anfield. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alitolewa nje wakati wa kipindi kwanza na kusababisha hali kuwa mbaya kwa kikosi chake na kupelekea kufungwa mabao 3-2 na mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu. 
Akihojiwa kuhusiana na hali ya nyota huyo, kocha wa City Manuel Pellegrini amesema itakuwa ngumu kwa mchezaji huyo kumaliza msimu huu. 
Toure alijiumiza mwenyewe baada ya kupiga shuti lililopaa katika mchezo huo wakati City wakijaribu kurejea baada ya kufungwa bao la kuongoza na Raheem Sterling.

No comments:

Post a Comment