STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 11, 2014

Wigan yaichimba mkwara Arsenal

MABINGWA watetezi wa Kombe la FA, Wigan Athletic wamesema hawatakuwa tayari kuona kombe hilo likitoweka mikononi mwao hususan watakapocheza mechi ya nusu fainali dhidi ya Arsenal kwenye Uwanja wa Wembley Jumamosi.
Wigan iliutwaa ubingwa huo msimu uliopita baada ya kuifunga Manchester City katika mechi ya fainali.
Hull City, ambayo haijawahi kufika nusu fainali, huku ikitinga hatua hiyo baada ya miaka 85 iliyopita, itacheza nusu fainali nyingine dhidi ya Sheffield United Jumapili.
Arsenal itavaana na watetezi hao wa FA wakiwa wanauguza kipigo cha aibu walichopewa na Everton katika pambano lao la mwisho la Ligi Kuu ya England dhidi ya Everton waliowatambia kwa kuwalaza mabao 4-0

No comments:

Post a Comment