STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 20, 2014

Madaktari wamuonya Ronaldo, mwenyewe mbishiiii

RIO DE JANEIRO, Brazil
DAKTARI wa Cristiano Ronaldo amemuonya nyota huyo wa Ureno kuwa, kama anajitia matatizoni kuichezea Ureno kwenye Kombe la Dunia kwa hali aliyionayo na  majeruhi na kwamba anaweza kushindwa kukipiga katika klabu yake kama ataendelea kucheza huko Brazil.
Nyota huyo wa Real Madrid anasumbuliwa na majeraha ya goti na yupo katika presha ya kuingoza timu yake kwenye mechi ya Jumapili dhidi ya Marekani baada ya mchezo wa ufunguzi wa kundi lao kukubali kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya Ujerumani.
Kwa mujibu wa gazeti la El Confidencial, daktari wa Mreno huyo Jose Carlos Noronha alimwambia Ronaldo (29), kuwa: 'Liache goti lako lipumzike, ama mustakabali wako wa baadaye uwe matatizoni', hata hivyo Ronaldo aliripotiwa kujibu: 'Mimi ndiye mwenye wajibu wa kusema nicheze ama ni sicheze'.
Ronaldo alipigwa picha akifanya mazoezi huku mguu ukiwa na 'bandeji' kwenye goti la kushoto linalomsumbua.
Kumekuwa na hofu kubwa kuhusu nyota huyo wa Real Madrid kuwa fiti wakati michuano hii ikiendelea, baada ya maumivu ya paja na goti kumlazimisha kutokuwamo wakati wa maandalizi ya michuano hiyo hapo awali.
Ronaldo alikiri kuwa fiti kwa asilimia 100  katika mechi ya ufunguzi ambayo walichapwa 4-0 na Ujerumani, hata hivyo pamoja na kukiri huko cheche zake hazikuonekana na kuweza kuisaidia timu yake kubadili matokeo.
Sasa inaonekana kuwa mshindi huyo wa Ballon d'Or anasumbiliwa na goti baada ya kuonekana akipatiwa matibabu wakati wakijifua huko Campinas, Brazil.
Ronaldo alitolewa nje kwa machela kabla ya kufungwa 'bandeji' pamoja na kuwekewa barafu mguuni katika goti la kushoto ikiwa ni dakika 30 kabla ya mazoezi kumalizika, hata hivyo hakuweza tena kurejea mazoezini hadi yalipomalizika.

No comments:

Post a Comment