STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 20, 2014

26 Stars waitwa kambini safari ya Botswana

WACHEZAJI 26 wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) wanatarajiwa kuingia kambini Jumatatu kwa ajili ya safari ya Gaborone, Botswana. 
Kwa mujibu wa Kocha Msaidizi wa Stars Salum Mayanga, wachezaji hao wanatakiwa kuripoti katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa safari hiyo inayotarajiwa kuwa Juni 24 mwaka huu, ikiwa ni maandalizi ya mechi ya kuwania Fainali za Afrika 2015 dhidi ya nchi ya Msumbiji (Mamba).
Wachezaji wanaoatakiwa kambini ni pamoja na makipa Deogratias Munishi 'Dida' na Aishi Manula, mabeki Benedictor Tinoko, Kelvin Yondani, Said Moradi, Nadir Haroub, Joram Nason, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Edward Charles, Aggrey Morris na Pato Ngonyani. 
Wengine ni viungo Frank Domayo, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said Juma, Haruna Chanongo na Himid Mao, huku washambuliaji wakiwa ni John Bocco, Simon Msuva, Kelvin Friday, Ramadhan Singano, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Mwegane Yeya.
Stars itavaana na Mamba Julai 20 jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana nao wiki mbili baadaye mjini Maputo Msumbiji na itakayopenya hapo itatinga kundi F la mchujo wa fainali hizo za Afrika za nchini Morocco.
Katika kundi hilo Stars ikifuzu itakumbana na timu za Zambia, Niger na Cape Verde.

No comments:

Post a Comment