STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 20, 2014

Filbert Bayi yachomoa kwenda kutetea taji la Netiboli Dodoma

MABINGWA watetezi wa Ligi Daraja la Kwanza kwa mchezo wa Netiboli, Filbert Bayi na Teachers za jijini Dar es Salaam hazitashiriki michuano hiyo itakayoanza rasmi mwezi ujao mjini Dodoma.
Hata hivyo klabu hizo zimetakiwa kutoa sababu maalum za kukwepa michuano hiyo ili kuepuka adhabu ya kushushwa daraja kama kanuni za ligi hiyo zinazovyoelekeza.
Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli (CHANETA), Anna Kibira aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa,  uongozi wa klabu hizo ulitoa taarifa za mdomo kwamba wasingeshiriki michuano hiyo ya Dodoma.
"Hata hivyo tuliwaambia waandike barua na kutoa sababu zinazoelewekwa ili kuepuka kukumbwa na 'rungu' la kanuni dhidi ya klabu zinazokacha michuano," alisema Kibira.
Aliongeza kuwa ukiondoa timu hizo, mpaka sasa klabu 17 zimethibitisha kushiriki ligi hiyo itakayoanza Julai 12-26.
Kibira alizitaja klabu zilizothibitisha ni JKT Ruvu, Jeshi Stars, CMTU, JKT Mbweni, Uhamiaji na Polisi Dar zote zikiwa za Dar es Salaam.
Nyingine ni Polisi, Magereza na TTL zote za mkoa wa Morogoro, Polisi-Kigoma, Polisi-Mbeya, Polisi-Arusha, Mbeya City Queens, CIDT-Arusha, Polisi-Shinyanga, Polisi-Dodoma, Polisi-Mwanza na Nyanyembe ya mkoa wa Tabora.
Kibira alisema maandalizi kwa ajili ya michuano hiyo kwa ajili ya kusaka bingwa na timu nne za kuiwakilisha Tanzania Bara kwenye Ligi Kuu ya Muungano yanaendelea vyema kwa sasa mjini Dodoma.
========

No comments:

Post a Comment