STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 12, 2014

Aisha Bui: Nilihatarisha maisha yangu kuwapa raha mashabiki wangu

NYOTA wa kike wa filamu nchini, Aisha Fat'hi 'Aisha Bui' amevunja ukimya na kuibuka na filamu mpya iitwayo 'Mshale wa Kifo' huku akiweka bayana kwamba alijitoa na kuhatarisha maisha yake kuiandaa filamu hiyo iliyotengenezwa porini.
Aisha alisema kuwa kutokana na maoni ya mashabiki wa filamu wanaolalamika kuwa filamu  nyingi za Bongo zimekuwa za mijini tu, huku baadhi ya matukio yakirudiwa kila katika sinema hizo hali hiyo ilimfanya abadilishe na kutoka kivingine.
Alisema hivyo aliamua kuhama mji na kwenda porini kuicheza filamu hiyo ambapo chupuchupu yeye na waigizaji wenzake kung'atwa na nyoka wakati wakiitengenza filamu hiyo.
“Nilijitoa na kuhatarisha maisha yangi kwa kuingia msituni ili tu kutengeneza filamu ambayo ikakata kiu ya mashabiki wasiovutiwa na filamu za 'sebuleni'. Ninajua nina deni kwa wapenzi wa kazi zangu, wanajua mimi ni bora hivyo lazima niwe bora kila mwaka,” alisema Aisha.
Filamu hiyo ya 'Mshale wa Kifo', imetengenezwa na kampuni ya Yuneda Entertainment ikiwashirikisha wakali kama Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’, Esha Buheti, Salim Ahmed ‘Gabo Zigamba’ na wasanii wengine.

No comments:

Post a Comment