STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 14, 2013

Chelsea yaipumulia Arsenal kileleni, Everton yaua

Fernando Torres and Willian
Torres akipongezwa baada ya kuifungia Chelsea
Leon Osman
Everton wakiwatungua Fulham

VIJANA Jose Morinho, Chelsea muda mfupi uliopita imepata ushindi muhimu wa mabao 2-1 ikiwa uwanja wa Stanford Bridge kwa kuicharaza Crystal Palace.
Bao la kwanza la Chelsea kutumbukiwa wavuni na Fernando Torres katika dakika ya 16 kabla ya Marouane Chamakh kuisawazishia wageni dakika ya 29.
Katika dakika ya 35 Ramires aliiongezea Chelsea bao la pili na kudumu hadi wakati wa mapumziko na hata kipindi cha pili kilipoanza matokeo yalibaki hivyo na wenyeji kuvuna pointi tatu na kukamata nafasi ya pili nyuma ya Arsenal waliopigwa mchana wa leo.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Everton walikwea hadi nafasi ya nne baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-1 wakiwa nyumbani dhidi ya Fulham,  huku Newcastle United ilibanwa nyumbani na kulazimishwa sare ya bao 1-1 na timu ya Southampton.
West Ham United nayo ikiwa nyumbani ililazimishwa suhulu ya bila kufungana dhidi ya Sunderland, ilihali Cardiff City ilipata ushindi wa kushtukiza wakiwa nyumbani kwa kuilaza West Brom kwa bao 1-0.
Hull City muda mchache uliopita imeanza pambano lake dhidi ya wageni wao Stoke City katika pambano jingine la kufungia dimba siku la leo kabla ya kesho kushuhudiwa kivumbi cha mechi nyingine tatu.

No comments:

Post a Comment