STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 14, 2013

Hatari! Ajali nyingine tena yaua wawili

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhx_WAjq_EmxNFNzmr5N_sdMyYNC6gHIbtlxBMjcrq-xftKzqgCZGe5YveNwrsZgN1zt03CdNE5FljeJzc5rJlQe-YDM3eDdlGPMS5dMtP3cLfnR-J_wcYBaeSyZE5ZLiv54gLEnsFGYNo/s1600/bunda+express+accident-kuninews+blog.jpg
Hii kati ya ajali ambazo zimekuwa zikitokea kila mara Tanzania
WATU wawili wamekufa na wengine 14 kujeruhiwa baada ya basi 
waliolokuwa wakisafiria la Simiyu Express kupinduka katika eneo la 
Ihumwa nje kidogo ya manispaa ya Dodoma.

Basi hilo lenye namba za usajili T 717 ANL aina ya scania basi lilikuwa
likiendeshwa na dereva aliyetambulika kwa jina la Mramba Issa (31).

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kaimu Kamanda wa Polisi
mkoani hapa Susan Kaganda, alisema kuwa basi hilo lilikuwa linatokea
Bariadi kwenda Dar es salaam likiwa na abiria 60 liliacha njia na 
kupinduka kutokana na mwendo kasi .
Kamanda alisema kwamba ajali hiyo ilitokea leo alfajiri majira ya saa tisa
usiku katika barabara ya Dodoma-Dar es salaam  eneo la Elshadai .
Kamanda Kaganda aliwataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni 
pamoja na dereva wa basi hilo Mramba Issa mkazi wa Magomeni 
Dar es salaam na Frola Erenest(21) Mwali wa shule ya msingi Mwamoto 
kolokolo, Bariadi.
Aidha kamanda akizungumzia zaidi ajali hiyo alisema kwamba basi hilo
lilikuwa likiwakwepa askari wa barabarani kwa kupita njia za panya.
Alifafanua kuwa kwa basi hilo kusafiri usiku huo ni kukwepa askari .
Aliwataka pia wamiliki wa magari kuweka madereva wawili kwa 
magari ya masafa marefu na pia wazingatie sheria za barabarani. 
HABARI LEO 

No comments:

Post a Comment