STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 14, 2013

Arsenal nyang'anyang'a kwa Manchester City

Yaya Toure akiwajibika uwanjani kuisaidia City kuiua Arsenal mabao 6-3

Kun Aguero akishangilia bao lake lililofungua kapu la mabao kwa Arsenal leo
MASHABIKI wa klabu ya Arsenal, vinara wa Ligi Kuu ya England leo watalala wakiota njozi mbaya baada ya timu yao kupokea kipigo cha aibu cha mabao 6-3 toka kwa Mancherster City katika mfululizo wa Ligi hiyo.
Wakicheza ugenini huku wakiwa wanaugulia kipigo cha mabao 2-0 walichopewa na Napoli ya Italia katika Ligi ya Mabingwa Ulaya,  vijana wa kocha Arsenal Wenger walishindwa kufurukuta kwa City waliokuwa uwanja wao wa Itihad.
Goli la mapema la Sergio 'kun' Aguero katika dakika ya 14 lilionyesha dalili mbaya kwa wageni japo winga aliyerejea tena dimbani, Tim Walcot alisawazisha bao hilo dakika ya 31 kwa pasi ya Mesut Ozil kabla ya Negredo kuongeza bao la pili dakika nane baadaye na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 2-1.
Fernandinho aliiongezea City bao la tatu dakika tano baada ya kipindi cha pili  kabla ya Walcot kurejea tena nyavuni kwa kuifunga Arsenal bao la pili dakika ya 63 akimalizia kazi ya Aaron Ramsey.
Hata hivyo jahazi la Gunners liliendelea kuzama ugenini kwa mara ya pili mfululizo baada ya David Silva kufunga bao la nne dakika tatu baadaye kwa pasi ya Juses Navas na Fernandinho kuongeza bao jingine dakika mbili kabla ya mchezo huo kuisha akimalizia pasi ya Samir Nasir.
Beki Pet M Mertesacker aliifungia Arsenal bao dakika ya nne ya nyongeza ya pambano hilo kabla ya Yaya Toure kupigilia msumari wa mwisho kwa kufunga bao kwa mkwaju wa penati dakika mbili baadaye katika muda huo wa nyongeza na kufanya mechi kuisha kwa mabao 6-3, Arsena ikiwa hoi.
Mechi nyingine zinaendelea hivi sasa katika ligi hiyo na MICHARAZO itaendelea kuwaleta.

No comments:

Post a Comment