STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 12, 2014

Van Gaal awaonyesha Chicharito, Nani mlango wa kutokea Man United

Mlango u wazi kwenu kutimka Old Traffiord
SIKU chache kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya England na kufungwa kwa pazia la usajili katikia ligi hiyo, Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amewaeleza wachezaji sita akiwamo beki wa kulia Rafael kwamba wanaweza kuchapa mwendo.
Marouane Fellaini, Wilfried Zaha, Nani, Shinji Kagawa na kinda yosso Will Keane pia wamevunja 'ndoa' na kikosi hicho cha Van Gaal na hilo limefanyika wakati United ikijifua katika Uwanja wa mazoezi wa  Carrington Jumamosi mchana.
Inaeleweka kuwa Mholanzi huyo amewaambia Fellaini, Zaha, Nani na Keane klabu hiyo itasikiliza ofa kwao baada ya kuwaweka sokoni rasmi.
Rafael, alishangaa kusikia jina lake likiwa katika orodha hiyo na kwamba pia anaweza kulazimisha kuondoka wakati huu klabu hiyo ikisaka beki wa kulia. Kagawa atatumika lakini kaelezwa ataanzia benchi nyuma ya Ander Herrera na Juan Mata.
Kiungo Anderson na mshambuliaji Javier Hernandez pia nao tayari wanajua kwamba United itasikiliza ofa endapo zitawasili mezani kwao. Southampton, Inter Milan, Tottenham, Atletico Madrid na Juventus zote zimeonyesha nia ya kumsajili Mmexico huyo, wakati Napoli itakuwa tayari kumsajili Fellaini kama dili hilo litakubalika na United.
Newcastle inaongoza katika vita ya kumsajili Zaha, huku Crystal Palace, West Ham na Nottingham Forest nazo zikihitaji huduma yake.
Cardiff City imeulizia uwezekano wa kumsajili kwa mkopo Keane ambaye ni pacha wa beki Michael, lakini United inahitaji kumtazama zaidi kabla ya kukamilisha dili hilo.
Kwa sasa United ipo sokoni ikisaka mabeki wapya wawili baada ya kushindwa kumsajili beki wa kati wa Arsenal, Thomas Vermaelen ambaye juzi alijiunga rasmi na Barcelona
Mabingwa hao wa zamani wamejipanga kufanya vyema katika msimu huu baada ya msimu uliopita kuboronga na kumaliza kwenye nafasi ya katikati tofauti na mazoea yao.

No comments:

Post a Comment