STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 2, 2014

Arsenal yamnyakua Welbeck wa Man Utd

http://articles.squarefootball.net/.a/6a00e5521030508834019104738508970c-pi 
KOCHA Arsene Wenger amefanya jambo la maana katika kutatua tatizo la safu yake ya ushambuliaji baada ya kukubali kumsaini kwa Pauni Milioni 16 mshambuliaji wa England, Danny Welbeck.
Kocha huyo wa Arsenal, alikuwa Italia kuthibitisha ahadi ya kucheza mechi hisani, ameonyesha hisani inaanzia nyumbani baada ya kuwapiga bao Spurs kwa kumsaini mshambuliaji huyo wa Manchester United.
Welbeck, anayeondoka Old Trafford baada ya kushindwa kumvutia kocha Louis van Gaal tangu Mholanzi huyo awasili msimu huu, awali alitolewa kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kwa Pauni Milioni 3.
Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 akalazimishwa kuuzwa moja kwa moja aka pate mwanzo mzuri mpya na kuisaidia Arsenal kuilazimisha United kupunguza bei kutoka Pauni Milioni 18 walizotaka awali kabla ya mchezaji huyo kusaini Mkataba wa miaka mitano.

No comments:

Post a Comment