STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 27, 2014

Simanzi! Nahodha, Kipa Bafana Bafana auwawa na majambazi

http://citizen.co.za/wp-content/uploads/sites/18/2013/10/TL_1081310-602x400.jpgNAHODHA na kipa tegemeo wa timu ya soka ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana, Senzo Meyiwa ameuwawa na Majambazi.
Taarifa kutoka nchini Afrika Kusini zilizotolewa na klabu yake ya Orlando Pirates zinasema kuwa kipa huyo alipigwa risasi akiwa nyumbani kwake Vosloorus Maili 20 Kusini mwa jiji la Johannesburs usiku wa jana.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa kipa huyo alikuwa na rafiki yake wa kike Kelly Khumalo msanii wa Pop aliyezaa naye mtoto mmoja hivi karibuni, licha ya kwamba kipa huyo alikuwa na ndoa yake. Inaelezwa kuwa watu watatu walivunja nyumba yake na wawili kuingia ndani na mmoja kusalia nje ambapoo waliwaamuru kuwapa simu za mkononi na kisha kupiga risasi ambazo zilimpaka kipa huyo kifuani
Inaelezwa kuwa kipa huyo aliyezaliwa SDeptemba 24, 1987 alifariki wakati akiwahishwa hospitalini.
Kupitia akaunti yao, klabu ya Orlando iliandika katika Twitter; ikielezwa kuhuzunishwa na kipa cha kipa na nahodha wao huyo huku Mwenyekiri wao, Irvin Khoza kuongeza kuwa ' Hii ni huzuni kubwa kumpoteza Senzo huzuni hii ni kwa familia yake hususani watoto wake kwa Orlarando Pirates na taifa klwa ujumla,"

No comments:

Post a Comment