STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 30, 2014

MSIBA! MZEE MANENTO WA BONGO MOVIE AFARIKI!


TASNIA ya sanaa imeendelea kukumbwa na majonzi baada ya msanii mwingine wa Bongo Movie, David Manento 'Mzee Manento' kufariki.
Mzee Manento aliyekuwa swahiba mkubwa wa marehEMU Steven Kanumba alifariki usiku wa jana baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kisukari pamoja na Presha akiwa na miaka 73.
Rais wa Shirikisho la Wasanii Tanzania, TAFF, Simon Mwakifwamba amethibitisha kufariki kwa Mzee Manento na kusema kuwa msiba wake upo nyumbani kwake Kigogo/Mburahati jijini Dar es Salaam
Mzee Manento atakumbukwa hasa kwa filamu alizocheza kiumakini na marehemu Kanumba. 
Baadhi ya filamu zilizomjengea jina kubwa ni pamoja na Fake Pastor, Dar to Lagos na Hero of the Church.
Marehemu Manento anayetokea mkoa wa Kilimanjaro ameacha watoto 9 na inaelezwa tangu alipofiwa na mkewe miaka michache iliyopita alikuwa mpweke kiasi cha kushindwa hata kula vizuri.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Amina.

No comments:

Post a Comment