STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 30, 2014

Robo Fainali ya Capital One hii hapa

VINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea imepangiwa kukutana na Derby County katika Robo Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One League) huku vijogoo vya London, Tottenham Hotspur wakipangiwa wabaya wao Newcastle United.
Newcastle waliifumua Spurs mabao 2-1 nyumbani mwishoni mwa wiki katika Ligi kabla ya usiku wa jana kuitemesha taji Manchester City kwa kuilaza mabao 2-0 katika Capital One.
Kwa mujibu wa ratiba ya hatua huyo,  Liverpool impangwa kucheza na FC Bournemouth na robo fainali ya mwisho itazikutanisha timu za Sheffield United.
Mechi hizo zitachezwa Desemba 16 na ratiba kamili iko hivi;
Tottenham vs Newcastle
Derby vs Chelsea
Bournemouth vs Liverpool
Sheffield vs Southampton

No comments:

Post a Comment