STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, October 15, 2014

Ronaldo alibeba Ureno, Ujerumani bado gonjwa Ulaya

http://i.ytimg.com/vi/TevIMI1W8NI/0.jpg
Ronaldo akishangilia bao lake lililoiua Denmark nyumbani kwao
http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2014/10/Screen-Shot-2014-10-14-at-23.54.46.png
Wachezaji wa Ireland wakishangilia bao lao la kusawazisha dhidi ya Ujerumani
http://www.theglobeandmail.com/sports/soccer/article21090950.ece/BINARY/w620/510260433_534397343.JPG
Mabingwa wa Dunia, Ujerumani wakihenyeka uwanjani dhidi ya Jamhuri ya Ireland
WAKATI Mabingwa wa Kombe la Dunia Ujerumani wakiwa hawajatulia, Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo usiku wa jana aliifungia timu yao ya Ureno bao pekee lililowapa ushindi dhidi ya Denmark uwanja wa ugenini katika mbuio za kuwania Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya Euro 2016.
Ujerumani inayouguza kichapo cha mabao 2-0 ilichopewa na Poland wikiendi iliyopita ilishindwa kulinda bao lake na kujikuta wakilazimishwa sare ya baoa 1-1 nyumbani na Jamhuri ya Ireland waliochomoa bao 'jioni'.
Ton Kroos aliiandikia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 71, lakini wageni walikaza msuli na kulirejesha dakika za nyongeza kupitia John O'shea na kufanya timu hizo kugawana pointi huku Poland wakilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Scotland ikiwa nyumbani.
Matokeo ya mechi nyingine ni kwamba Ureno ikiwa ugenini iliizabua Denmark kwa bao 1-0 lililofungwa na nahodha wake Cristioano Ronaldo katika dakika ya lala salama mashabiki wakiamini kuwa timu hizo zimetoka suluhu na kuifanya Ureno kufikisha jumla ya pointi tatu na kushika nafasi ya tatu.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, Gibraltar imeendelea kutoa takrima baada ya kugongwa nyumbani mabao 3-0 na Georgia, San Marino kulazwa mabao 4-0 nyumbani na Uswisi, wakati Visiwa vya Faroe walilala nyumbani pia kwa bao 1-0 kutoka kwa Hungary, Finland ikafa pia nyumbani kwa mabaop 2-0 kw akipigo cha Romania na Ugiriki ikaendeleza unyonge kwa timu zilizocheza nyumbani jana kwa kulazwa mabao 2-0 na Ireland ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment