STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, October 15, 2014

Suarez akiri ilikuwa vigumu kukiri kosa la kumng'ata Chiellini

http://vertienteglobal.com/wp-content/uploads/2014/06/luis-suarez-anota-gol.jpghttp://img2.timeinc.net/people/i/2014/news/140707/luis-suarez-600.jpgSTRIKA nyota wa Barcelona, Luis Suarez amesema ilikuwa ngumu kukubaliana na ukweli wa kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la dunia nchini Brazil. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay aliyejiunga na Barcelona akitokea Liverpool kwa kitita cha Pauni Mil. 75 alifungiwa miezi minne kutokana na tukio hilo. 
Akihojiwa strika huyo amesema alikuwa akiona vigumu kukubali alichokifanya kwani yeye ni binadamu kama walivyo wengine. 
Suarez, 27, amesema alikuwa hataki kumsikiliza yeyote au kuongea na yeyote kwa sababu alikuwa hataki kukubaliana na ukweli. 
Suarez alimuomba radhi Chiellini Juni 30 zikiwa zimepita siku sita toka afanye tukio baada ya Uruguay kushinda bao 1-0 dhidi ya Italia, msamaha ambao ulipokelewa na beki huyo na kueleza matumaini yake kama Shirikisho la Soka Duniani-FIFA lingeweza kumpunguzia adhabu hiyo. 
Kabla kuomba radhi Suarez alikanusha kwa kudai kuwa aliteleza bahati mbaya na usoni mwa Chiellini na kumuangukia jambo ambalo lilikuwa kama vichekesho kwani tukio hilo lote lilionekana katika picha za video.

No comments:

Post a Comment