STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 3, 2014

Arsene Wenger awaonya wachezaji kuhusu Mitandao ya Kijamii

http://www.whoateallthepies.tv/EMP-6272392.jpg
Arsene Wenger
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini ni juu ya wachezaji kuchambua kile wanachoandika wakati wakituma ujumbe wao katika mitandao ya kijamii.
Kauli hiyo ya Wenger imekuja baada ya mshambuliaji wa Liverpool Mario Balotelli kuomba radhi kwa ujumbe aliochapisha ambao ulionekana kama wa kibaguzi.
Akihojiwa Wenger amesema jambo kubwa wanalofanya ni kuwaonya athari zake lakini hakuna anaweza kuwalinda saa 24 kwa siku. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wachezaji wenyewe wanapaswa kuwajibika na kuelimika jinsi ya kudhibiti wanachokiongea.

No comments:

Post a Comment