STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 7, 2014

Man United yamhakikisha LVG fedha za usajili mpya zipo

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02911/Louis_van_Gaal_2911698b.jpgKOCHA wa klabu ya Manchester United, Louis Van Gaal amehakikishiwa kupewa fedha za kufanya usajili kwenye kipindi cha Majira ya Kiangazi ili kuimarisha kikosi chake.
Uongozi wa klabu hiyo wamemueleka LVG kuwa pesa siyo tatizo kama akiamua kuimarisha kikosi chake katika kipindi cha majira ya kiangazi. 
Van Gaal alitumia kitita cha paundi milioni 150 katika majira ya kiangazi, ukiwemo usajili uliovunja rekodi Uingereza wa paundi milioni 59.7 kwa ajili ya Angel Di Maria lakini bado wanaburuzwa na vinara Chelsea kwa tofauti ya alama 11 katika msimamo wa Ligi Kuu. Kiungo wa ulinzi Kevin Strootman na mabeki Mats Hummels na Diego Godin wote wako katika rada za United. 
Hata hivyo, Ofisa Mkuu wa United Ed Woodward tayari ameshweka wazi kuwa hatataka kuchukua mchezaji kwa mkopo katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo Januari. 
Woodward alibainisha mwezi uliopita kuwa tayari wana wachezaji waliowalenga kwa ajili ya usajili ujao wa majira ya kiangazi ila yoyote atakayeweza kupatikana Januari watafanya mipango ya kumchukua.

No comments:

Post a Comment