STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 7, 2014

AC Milan yapigwa kidude ugenini

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/1130/fc_milan_jc_1296x729.jpg&w=738&site=espnfcMABINGWA wa zamani wa Italia na Ulaya, AC Milan jioni ya leo imedonyolewa ugenini bao 1-0 na Genoa katika mfululizo wa Ligi ya Italia Serie A.
Bao pekee lililowazamisha vijana wa Phillip Inzaghi 'Pippo' lilitumbukizwa wavuni katika dakika ya 32 na beki wa Genoa Luca Antonelli.
Kipigo hicho kimeifanya Milan kusalia nafasi ya saba ikiwa na pointi 21 wakati wenyeji wao wakipanda hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 26.
Katika mechi  nyingine zilizochezwa leo Napoli ikiwa nyumbani iling'ng'aniwa na Empoli na kutoka sare ya mabao 2-2, Atalanta ikaifumua Cesena kwa mabao 3-2  na Parma ikakubali kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Lazio.      

No comments:

Post a Comment