STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 7, 2014

Kumekucha Tamasha ya Dar Filamu 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLcamPrzOPqAwvFp6SOjwlxLD3rvs3Yew-V6frniQ6-Xn8Z3Wpbjq7k_PHVnYJwQyolBsv3T6sba6tDg2ENJ7iYIz0V8IxEpfAA5EZJw6JFDjRzZEiTIyybgcI8EBaqotLS6eYpt-vtNo/s1600/unnamed+(4).jpgTAMASHA la pili la Filamu la Dar es Salaam (Dar Filamu Festival 2014) linaratajiwa kufanyika kati ya Desemba 19-21 jijini Dar es Salaam na washiriki waliokuwa hawajajitokeza kuomba kushiriki wanatakiwa kufanya hivyo kabla ya kesho saa 10 jioni.
Mmoja wa waratibu wa tamasha hilo ambalo ni maaluma kwa kutangaza kazi za wadau mbalimbali wa filamu mbali na semina mbalimbali zinazoendeshwa juu ya namna ya kuzalisha filamu bora, Myovela Mfaiswa aliliambia MICHARAZO kuwa tamasha lao litafanyikaia viwanja vya Chuo cha Posta, KIjitonyama.
Mfaiswa alisema walitoa muda mrefu kwa washiriki kujitokeza kwa ajili ya ushiriki wa tamasha hilo na mwisho ni kesh Desemba 8 kabla ya kupangwa ratiba ya namna tamasha hilo litakavyoendeshwa kwa siku hizo tatu mfululizo.
"Tamasha leo linatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kati ya Desemba 19-21 na siku ya Jumatatu (kesho) ndiyo mwisho wa washiriki kujitokeza kama tulivyoanisha njia mbalimbali za kujiandikisha kwa kujaza fomu iliyopo kwenye mtandao wa www.filamucentral.co.tz na kwingineko," alisema Mfaiswa.
Mfaiswa alisema tamasha la mwaka huu pia litakuwa na mabalozi wake kama ilivyokuwa mwaka jana kwa waigizaji nyota, Vincent Kigosi 'Ray' na Elizabeth Michael 'Lulu' waliobeba jukumu hilo.

No comments:

Post a Comment