STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 7, 2014

Shamsa Ford kufungua mwaka na 'Mama Muuza'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGYUQewjSfxvYImYYUqeqR5s4zKjOWq18PYY-DuBI8lA3RzxLZBec1QNYfhVy9SwJB3SOuIUhel6gJ4SjEetukwoD7JgVTz7sBmnPBDh_u-X_YikEiCnC5es419mTWWc16yuaz4ZFgtrg/s1600/After+Death.JPG
Shamsa Ford katika pozi
 BAADA ya kuteka nyoyo za mashabiki kwa mwaka 2014 kupitia filamu yake mwenyewe iitwayo 'Chausiku', muigizaji nyota wa filamu nchini, Shamsa Ford anatarajiwa kuufungua mwaka mpya na 'Mama Muuza'.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku', filamu ya 'Mama Muuza', pia  ameiandika mwenyewe na kutamba itakuwa kali na 'funika bovu' kuliko kazi hiyo ya awali.
Shamsa alisema ndani ya filamu hiyo ambayo ndiyo itakayomfungulia mwaka 2014 ameigiza na wasanii mbalimbali akiwamo Baba Haji ambaye pia alikuwamo katika 'Chausiku'.
http://www.bongocinema.com/images/casts/Shamsa_Ford_03.jpg
Mkali Shamsa Ford
"Baada ya Chausiku kunifungia mwaka 2014, natarajia kuufungua mwaka mpya wa 2015 na kazi mpya iitwayo 'Mama Muuza' ambayo humo nimefanya makubwa kuliko hata yale ya 'Chausiku'," alisema.
Katika filamu ya 'Chausiku' moja kati ya filamu mbili alizocheza mwaka huu, nyingine ikiwa 'Hukumu ya Ndoa Yangu', Shamsa amecheza kama 'demu mcharuko' na kustaajabisha wengi tofauti na haiba yake ya upole.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgn06H7No1Bn4gEy1LuuHo_4kxOESMdn7FfRCRjWx2opt1DZbvduTi4LxKvsTLnceNFspO8SeueIjaoTLt3zuAD9FYRCrXAuc5KE1IOV9MvboGAFwEDmrc4t8Nwf6yzs_MUfOlKhzGsb64/s640/1.jpg
Shamsa Ford
Shamsa alidokeza filamu hiyo imesharekodiwa na kukamilika na kwa sasa inawekwa kwenye foleni kwa ajili ya kuingia mtaani mwakani na kuwataka mashabiki wake kusubiri uhondo huo

No comments:

Post a Comment