STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 16, 2015

Polisi Zanzibar, KMKM yaendeleza uteja Afrika

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi59R0MYcrxWHLeSNnC_vM50rvpo6pW4S079-xz073BM1qMzHu78BZ3M2A6-Rcffg0AKuCNlGJTx77XuEspNUQTYpSZxeIwClivBXmTswWbLyuGBKDZoXuu3mnXKpUwrCIZ62qjbxpxVhkw/s640/4.jpg
KMKM waliokufa 2-0 Sudan
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLCWb5BqldkVTcFvaO8san-9Nhbw4RdsAVAbuN1u3556K_TvVv67OvOYjoXCPZ7VpusnafOOpJiS6SLaDK-7wNEixcgcnDUbt54qaR2jof0UEU-xKJdBd0IUmCqdrNsyokdr0MSy0kmIY/s1600/IMG_3886.JPG
Polisi waliopigwa 'mkono' nchini Gabon
WAKATI wawakilishi wa Tanzania Bara, Azam na Yanga wakiwapa raha mashabiki wao, KMKM na Polisi Zanzibar zimeendelea kuwasononesha mashabiki wa soka wa visiwa hivyo baada ya kugeuzwa 'urojo' katika mechi zao za kimataifa zilizochezwa mwishoni mwa wiki.
Polisi wanaoiwakilisha Zanzibar kwenye Kombe la Shirikisho Afrika kama Yanga, ilikutana na kipigo cha mabao 5-0 toka kwa Moumana ya Gabon wakati mabingwa wa visiwani, KMKM wakilala 2-0 nchini Sudan kwa Al Hilal na kujiweka katika mazingira magumu ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Tangu Zanzibar ilipopata uanachama wa Shirikisho la Soka Afrika CAF, 2004, imekuwa ikifanya vibaya kwenye uwakilishi wa klabu kwa timu zao kuondolewa hatua za awali.
KMKM na Polisi maarufu kama Wazee wa Tunisia' watakuwa na mtihani mgumu swa na kupanda mlima mrefu kuweza kuzitoa Mounana na Al Hilal katika mechi zao za marudiano wakati wakiwa nyumbani.
Hiyo ni tofauti na wawakilishi wa Tanzania Bara, Yanga na Azam wenye kazi nyepesi kwenye mechi zao za marudiano wiki mbili zijazo ugenini dhidi ya timu za BDF XI ya Botswana na El Merreikh ya Sudan.
Yanga ilianza kwa kuizabua BDF kwa mabao 2-0 juzi kwenye Kombe la Shirikisho, kabla ya Azam kufuata mkumbo huo kwa kuilaza El Merreikh kwa idadi kama hiyo jana kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Matokeo mengine ya michuano ya hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika yapo hivi;
Al Ahli Tripoli     1 - 0     Smouha
COB     2 - 0     Moghreb Tétouan        
Raja Casablanca     4 - 0     Diables Noirs
St Michel United     1 - 1     Mamelodi Sundowns       
KCCA     1 - 0     Cosmos de Bafia        
Gor Mahia     1 - 0     CNaPS Sport        
Al-Malakia     0 - 2     Kano Pillars  
Recreativo do Libolo  3 - 1     Sanga Balende      

Mangasport     1 - 0     Bantu         
LLB Académic     0 - 0     Kabuscorp        
Séwé Sport     1 - 2     Kaloum Star
Real de Banjul     1 - 1     BYC
Pikine     1 - 0     Etoile Filante
MC El Eulma     1 - 0     Kedus Giorgis
Kaizer Chiefs     2 - 1     Township Rollers
Fomboni Club     0 - 1     Big Bullets
Azam     2 - 0     Al Merreikh 
Enyimba     3 - 0     Buffles de Borgou
Liga Muçulmana     0 - 0     APR
Mbabane Swallows     1 - 1     ZESCO United
USM Alger     3 - 0     Foullah Edifice
Al Hilal Omdurman     2 - 0     KMKM
Matokeo ya Kombe la Shirikisho Afrika;
Al-Ghazal     0 - 1     Petrojet
URA     3 - 2     Elgeco Plus
Benfica Luanda     2 - 0     Le Messager Ngozi
RSB Berkane     2 - 1     Onze Créateurs
Petite Rivièr…     1 - 2     Ferroviário Beira
Côte d'Or     2 - 3     Dedebit
RC Bobo-Dioulasso     0 - 1     Warri Wolves
Volcan Club     0 - 1     Petro de Luanda
Young Africans     2 - 0     BDF XI
Panthère     0 - 1     Rayon Sports
MC Alger     0 - 0     Sahel 
Leones Vegetar…     1 - 0     Dolphins
Étoile du Congo     1 - 2     FC MK
BV Wits     3 - 0     Royal Leopards
Khartoum 3     1 - 0     Power Dynamos
Sofapaka     1 - 2     Platinum
Al-Ittihad     6 - 1     Elect-Sport
Unisport Bafang     1 - 0     Olympique Ngor
Mounana     5 - 0     Polisi
Hearts of Oak     1 - 0     Police
Togo Port     2 - 0     CARA Brazzaville
ASO Chlef     2 - 0     Kamboi Eagles
Horoya     1 - 0     Fassell

No comments:

Post a Comment