STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 16, 2015

Shamsa Ford 'awauma' sikio wenzie, msikie...!

Kimwana Shamsa Ford
SHAMSA Ford ambaye ameufungua mwaka kwa kuuza sura ndani ya filamu ya 'Kudra' amewataka wasanii wenzake wa kike kujipanga mwaka 2015 ili kuhakikisha wanafika mbali kimataifa.
Shamsa anayejiandaa kupakua filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' alisema kuwa mwaka 2015 uwe mwaka wa mipango kwa wasanii wa filamu nchini hasa wa kike kwa kuhakikisha wanakuwa namba moja badala ya kuridhika na nafasi walizonazo.
Mwanadada huyo alisema kwa upande wake amejipanga kuhakikisha anafanya kila jitihada ili kung'ara ikiwamo kunyakua tuzo kwa vile uwezo na sababu ya kufanya hivyo anayo.
"Ningependa kuwakumbusha wasanii wenzangu wa kike kuamka na kuufanya mwaka 2015 uwe wa mwaka wa mafanikio kwao, tujipange tuweze kuona tunatamba kimataifa," alisema.
Shamsa aliyekimbiza mwaka jana kupitia filamu kadhaa ikiwamo 'Hukumu ya Ndoa Yangu' na ile yake ya 'Chausiku', alisema imefika wakati wasanii nchini waelekeze nguvu zao kwenye soko la kimataifa badala na kuridhika na mafanikio ya nyumbani

No comments:

Post a Comment