STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 16, 2015

Yamoto Band kwenda kutumbuiza kwa Malkia Elizabeth II

Kundi la Yamoto Band
Bango la onyesho hilo la Yamoto kwa Malkia
KUNDI linalofanya vizuri katika muziki wa kizazi kipya nchini, Yamoto Band, linatarajiwa kwenda nchini Uingereza kwa ajili ya kutumbuiza.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Said Fella, alisema Yamoto itaondoka nchini kesho kwa ajili ya kufanya onyesho lao siku ya Jumamosi.
Fella alisema onyesho lao litafanyika kwenye ukumbi wa Royal Regency, jijini London ikiwa ni mara ya kwanza kwa Yamoto kutua kwenye nchi hiyo ya Malkia.
Fella alisema ziara yao imeandaliwa na baadhi ya Watanzania wanaoishi Uingereza na taarifa walizonazo watafanya onyesho Februari 21 na kama kutakuwa na onyesho jingine la ziada watafahamu huko huko.
"Bendi itaondoka Febaruari 17 na onyesho litafanyika Februari 21 mjini London kwenye ukumbi wa Royal Regency," alisema Fella.
Kundi la Yamoto linaundwa na wasanii wanne wakali ambao ni Aslay, Maromboso, Enock Bella na Beka na limekuwa likitamba na nyimbo mbalimbali zikiwamo 'Yamoto', 'Nitajuta', 'Niseme', 'Tulia' na sasa wanatingisha na 'Nitakupwelepweta'

No comments:

Post a Comment