STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 11, 2015

Arsene Wenger awashushua wapambe nuksi

http://xmedia-nguoiduatin.cdn.vccloud.vn/149/2014/8/12/Arsene%20Wenger.jpg
BAADA ya kuanza Ligi Kuu ya England kwa kipigo cha nyumbani cha mabao 2-0 kutoka kwa West Ham United, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amewashushua wanaolazimisha afanye usajili ili kuimarisha kikosi chake kwa kusema huwa hakurupuki.
Wenger amesema kuwa hatakurupuka kukimbilia sokoni kutafuta wachezaji wapya kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili wa kiangazi baada ya kipigo cha kushtusha walichopewa.
Kipa Petr Cech ndio sura mpya pekee iliyotua Emirates katika kipindi hiki cha usajili na ameonekana kuanza vibaya kibarua chake hicho toka atoke Chelsea.
Kuna tetesi kuwa Wenger ameshatenga fungu kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema.
Lakini meneja huyo amesema hatakurupuka kusajili kwasababu ya kupoteza mchezo wao kwanza katika ligi kwani jambo la msingi ni kuangalia walipokosea na kurekebisha.

No comments:

Post a Comment