STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 11, 2015

Depay ajiapiza kuhusu jezi No. 7

http://images.thepeoplesperson.com.s3-eu-west-1.amazonaws.com/wp-content/uploads/2015/06/12150615/memphis.jpg
Depay
UKISIKIA kujishtukia ndiko huku, Mshambuliaji Mpya wa Manchester United, Memphis Depay amesem ana uhakika kuwa ataweza kuitendea haki jezi namba namba aliyopewa na klabu hiyo kama nyota wengine waliowahi kuivaa.
Depay alipewa namba hiyo mashuhuri baada ya Angel Di Maria kuondoka kwenda PSG na kufuatia nyayo za nyota wengine waliowahi kuvaa jezi kama Cristiano Ronaldo, David Beckham, Eric Cantona na George Best.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi amesema yuko tayari kuitendea haki jezi hiyo kama ilivyokuwa kwa nyota wengine na kutamba kuwa atafanikiwa akiwa Old Trafford.
Depay aliendelea kudai kuwa anafahamu changamoto yake na historia lakini ana uhakika ataendelea kuimarika zaidi na kupata mafanikio kama ilivyokuwa kwa wengine.
Manchester ilianza Ligi Kuu ya England kwa kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspur kwa bao la kujifunga la beki wa Spurs Kyer Walker.

No comments:

Post a Comment