STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 11, 2015

Yaya Toure aibeba Man City, ikishinda ugenini

Yaya Toure akifunga moja ya mabao yake usiku wa jana kuisaidia Manchester City kushinda ugenini mabao 3-0
http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/494/423/hi-res-b27d356a2da129aaa8e144db5c571976_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75
Vincent Kompany akishangilia bao lake lililokuwa la tatu kwa Man City
Ivorian midfielder Toure wheels away in celebration as Fernandinho congratulates his team-mate for the early strike
Oyooo Oyoooo! Man City wakishangilia mabao yao jana usiku
MANCHESTER City imeanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu ya England baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya West Bromwich.
City ilipata ushindi huo usiku wa kuamkia leo, huku Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure akifunga mabao mawili na kuipeleka timu yake kileleni mwa msimamo baada ya raundi ya kwanza.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure aliyefunga alianza kuifungia Manchester City dakika ya tisa baada ya shuti lake la umbali wa mita 20 lililombambatiza Boaz Myhill na kutinga nyavuni, kabla ya kufunga la pili dakika ya 24.

Nahodha wa Man City, Vincent Kompany akakamilisha ushindi mnono katika mchezo wa kwanza wa timu yake kwa kufunga bao la tatu dakika ya kwa kichwa 59.  

Mchezaji mpya, Raheem Sterling aliyesajiliwa kutoka Liverpool, alicheza vizuri katika kikosi cha City jana, lakini akapoteza nafasi nzuri na ya wazi ya kufunga.

No comments:

Post a Comment