STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 3, 2015

Uchafu waikwaza Rio de Jeneiro Olimpiki 2016

Maeneo ya Fukwe za Rio De Jeneiro yatakayofanyika mashindano ya Olimpiki ya mwakani

Rais wa Kamati Kuu ya Kimataifa ya Olimpiki (OIC), Thomas Bach, amesema kuwa uchafuzi wa bahari ni moja ya kikwazo kwa jiji la Rio de Janeiro, Brazili katika maandalizi ya michuano ya hapo mwakani.
Hata hivyo kutokana na hali hiyo waandaji wa mashindano hayo ya riadha wamesema kuwa watafanya kila linalowezekana kwa afya ya wanariadha wakati wa Olympiki.
Takribani asilimia 70 ya maji taka yanamwagika Rio de Janeiro katika fukwe za Guanabara,eneo ambalo wapiga mbizi watafanyia mashindano yao.
Katika hali inayoonyesha ni hatari kwa afya wanariadha walioko kwenye mafunzo katika pwani hiyo wameona mizoga ya wanyama na uchafu ukiwa ukingoni mwa eneo hilo ambalo mashindano hayo yatafanyika.

No comments:

Post a Comment