STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 10, 2010

Kanumba, apania uzinduzi wa Off Side DR Congo



NYOTA wa filamu nchini, Stephen Kanumba, ametamba kuwa uzinduzi wa kazi mpya aliyotoa pamoja na Vincent Kigosi 'Ray' iitwayo 'Off Side' utakaofanyika wiki ijayo nchini DR Kongo, utakuwa wa aina yake kutokana na jinsi walivyojiandaa kuwapa raha mashabiki wao nchini humo.
Uzinduzi wa filamu hiyo iliyowarejesha tena wawili hao pamoja tangu walipotoa Ophra miaka miwili iliyopita, unatarajiwa kufanyika kati ya Desemba 15-20 katika miji miwili ya nchi hiyo ya Goma na Bukavu.
Akizungumzia uzinduzi huo, Kanumba, alisema wamepania kufanya kweli ili kusuuza nyoyo za mashabiki wao lukuki waliopo katika nchini hiyo na Ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati na pia kutaka kujitengenezea majina yao katika anga la kimataifa.
"Hii ni nafasi ambayo haipaswi kuichezea na ndio maana tunaenda kamili kuwapa raha mashabiki wetu wakati wa uzinduzi huo, ili kujitangaza kimataifa," alisema Kanumba.
Kanumba, atakayeambatana na washiriki vinara wa filamu hiyo, Ray, Irene Owoya, Aunty Ezekiel na mtoto Jennifa aliyecheza filamu za This is It na Uncle JJ, alisema maandalizi yao ya kwenda kufanya uzinduzi huo yamekamilika na kwamba wakati wowote wiki ijayo watatua nchini humo kufanya mambo.
"Tunaendelea vema na maandalizi ya shughuli hiyo na tunawasihi wakazi wa Kongo wakae mkao wa kula kupata klitu roho inapenda kqwani tutafanya onyesho la jukwaani la dakika kama 30 ili kukonga nyoyo zao," alisema.
Katika filamu hiyo ya kimapenzi, Kanumba amecheza kama kijana maskini anayelazimishwa mapenzi na mke wa tajiri kitu ambacho kinamletea kizaazaa cha aina yake.
Kanumba alisema mara baada ya uzinduzi huo wa Kongo wataenda Burundi kabla ya kurejea nchini kwa ajili ya kuitoa hadharani kupitia kampuni ya Steps Entertainment ambayo ndiyo yenye kibali cha kuisambaza kazi hiyo.

No comments:

Post a Comment