STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 10, 2010

Dance Music Competition laiva

USAILI wa wasanii chipukizi wa muziki wa dansi watakaoshiriki shindano la kusaka nyota wapya wa muziki huo nchini, kupitia shindano la 'Dance Music Competation' unatarajiwa kuanza rasmi Desemba 20-21 kwenye ukumbi wa Afri Center, Ilala jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa shindano hilo, Seleman Mathew alisema maandalizi ya mchakato huo umeshaanza kwa kuanza kutoa fomu za ushiriki kwa wanaopenda kushiriki mchuano huo kuzichangamkia kabla ya usaili huo utakaoendeshwa na majaji wanne.
Mathew aliwataja majaji hao kuwa ni wanamuziki wakongwe wa muziki huo nchini, Ally Choki wa Extra Bongo, Tshamanga Kalala Assosa wa Bana Marquiz, Nyota Waziri wa Kilimanjaro Band 'Wana Njenje' na Abdul Salvador 'Father Kidevu' wa Hisia Kali Band.
'Mchujo wa kusaka vijana kwa ajili ya shindano letu na nyota wapya wa muziki wa dansi utaanza rasmi Desemba 20-21 kwenye ukumbi wa Afri Center Ilala kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 11 jioni, na watakaopenya wataingia kwenye kinyang'anyiro hicho," alisema Mathew.
Alisema kinyang'anyiro cha shindano hilo kitaanza Januari 16 kwa washiriki kuingia kambini na kupigiwa kura hadi atakapopatikana mshindi katika fainali zitakazofanyika Machi 6 mwakani.
Mathew, beki za zamani wa timu za Simba, Yanga, Plisner na Ndovu-Arusha, alisema lenye lengo la shindano hilo ni kuibua wanamuziki wapya wa dansi na kuendeleza muziki huo nchini kuwabadili vijana wengi kuona hakuna muziki mwingine zaidi ya Bongofleva tu.
Alisema washiriki wanaotaka kushiriki wanapaswa kuwa katika kundi la kuanzia wasanii watano hadi saba wenye uwezo wa kuimba nyimbo za muziki wa dansi na kuongeza kwa wale ambao hawana makundi pia wanaruhusiwa muhimu wawe na uwezo katika muziki huo.
Alisema fomu za ushiriki wa shindano hilo zinapatikana kwenye ukumbi wa Afri Center kwa gharama ya Sh 3,000 na kuwataka wenye vipaji hivyo kuchangamkia nafasi hiyo, huku akiwataka wadhamini kujitokeza kuwapiga tafu kufanikisha shindano hilo la kwanza nchini kwa muziki huo.

No comments:

Post a Comment