STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 10, 2010

Munishi aja kuchangia yatima Bongo



MUIMBAJI nyota na mkongwe wa muziki wa Injili, Faustin Munishi anayeishi Kenya, anatarajia kutua nchini wiki ijayo kwa ajili ya kuja kutumbuiza kwenye tamasha maalum la muziki wa Injili la kuchangisha fedha kwa ajili ya yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Tamasha hiloi litakalofanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama siku ya Desemba 26, limeandaliwa na asasi ya Keep a Child Alive, ambapo wasanii mbalimbali wa muziki wa injili wa ndani ya nje ya nchi wamealikwa kuja kulipamba.
Mratibu wa tamasha hilo, Godfrey Katunzi, aliiambia MICHARAZO kuwa, kati ya wasanii wa muziki wa Injili watakaotumbuiza siku hiyo ya 'Boxing Day' ni muimbaji mkongwe, Mtanzania Faustin Munishi, ambaye kwa miaka mingi anafanya shughuli zake nchini Kenya.
Katunzi, alisema mbali na Munishi anayetamba na vibao kama Chini ya Mwamba, Paulo na Sila, Amua Mwenyewe, Nimuogope Nani na nyingine, wengine watakaotumbuiza siku siku hiyo ni Dk Aaron, Jane Misso, Beatrice Muone na kwaya mbalimbali za jijini Dar es Salaam.
Mratibu huyo ambaye ni Katibu wa asasi hiyo ya Keep a Child Alive, alizitaja baadhi ya kwaya hizo ni ile ya New Life Church wanaotamba na albamu yao ya 'Sipati Picha', Tabata Menonite maarufu kama Wakunyatanyata na nyinginezo.
Katunzi alisema, lengo la tamasha hilo la injili ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia yatima na watoto hao wa mitaani walipiwe ada na kununuliwa vifaa na sare za shule pamoja na kutatua matatizo mbalimbali waliyonayo.
Aliwaomba watu binafsi na makampuni yenye uwezo kujitokeza kuwapiga tafu katika tamasha hilo, ili kutimiza malengo la kuwaonyesha upendo watoto hao, akidai jukumu la kusaidia na kulea yatima ni la watu wote bila kujali, dini, rangi, kabila au jinsia.

No comments:

Post a Comment