STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 10, 2010

Levent kurekodi tatu mpya

BAADA ya ukimya mrefu tangu ilipofyatua albamu yao ya pili ya Mama Kabibi, bendi ya muziki wa dansi ya Levent Musica ya mjini Morogoro wiki ijayo itaingia studio kurekodi nyimbo tatu kwa ajili ya maandalizi ya albamu yao ijayo mpya.
Kiongozi wa bendi hiyo, Seleman Ramadhani 'Suzuki Sauti ya Malaika', aliiambia MICHARAZO jana kuwa nyimbo zitakazorekodiwa ni 'Pongezi Baba Madinda' na 'Mapenzi Maradhi' alizotunga yeye (Suzuki) na 'Mapenzi Sio Pesa' wa Steve Dokta.
Suzuki, alisema nyimbo hizo ni katyi ya nyimbo sita mpya za bendi hiyo zilizopangwa kurekodiwa kwa ajili ya albamu yao mpya na ya tatu ambayo wamepanga kuitoa mapema mwakani.
"Tupo katika maandalizi ya kwenda kurekodi nyimbo mpya tatu, tukiwa tunajiandaa kupakua albamu yetu ya tatu, kwa kweli kwa sasa Levent tupo kamili na tumepania," alisema Suzuki.
Mtunzi na muimbaji huyo, aliyerejea katika bendi hiyo baada ya kuikimbia kwa muda na kujiunga na Extra Bongo, alisema nyimbo nyingine tatu zimeshaanza kufanyiwa mazoezi na mara baada ya kumaliza kurekodi hizo za awali watarejea tena studio kukamilisha nyimbo hizo.
Kuhusu kikosi chao, Suzuki alisemakipo kamili, kila idara kuanzia safu ya unenguaji, wapiga ala na waimbaji ambao mbali na yeye yupo pia Steve Dokta na Salum Mzalamo 'Baba Mapacha'.
Bendi hiyo ya Levent ilianzishwa mwaka 2004 na imewahi kufyatua albamu mbili tu hadi sasa ambazo ni Rafiki ya 2006 na ile ya Mama Kabibi ya mwaka 2008 wakati bendi ikiwa chini ya Richard Malifa, alioyewahi kung';ara na bendi mbalimbali hapa nchini.

No comments:

Post a Comment